Posted by : Unknown Sunday 27 July 2014


pix_1402578975e131615_1 

Huu unaweza sio mwaka mzuri kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Cameroon Samuel Eto’o, baada ya timu yake ya taifa kufanya vibaya kwenye michuano ya kombe la dunia, na akiwa hana timu ya klabu ya kuichezea baada ya kumaliza mkataba wake na Chelsea, sasa amefunguliwa kesi nzito mahakamani.

 Kesi hizo za udhalilishaji kwa kusambaza picha za utupu, vitisho, ununuzi/uuzaji wa binadamu, udanganyifu, na vitisho zimefunguliwa kwenye mahakama moja jijini Yaounde, Cameroon, na aliyekuwa mchumba wa mshambuliaji wa huyo za zamani wa Chelsea, Hélène Nathalie Koah.

Mapema wiki iliyopita Koah alifungua kesi hizo dhidi ya Eto’o ambaye amekana mashtaka hayo.
Hatua hiyo ya imekuja siku chache baada ya kusambaa kwa picha zake za utupu kwenye mtandao Facebook, ambazo mhudumu huyo wa zamani wa ndege amesema zimesambazwa na Eto’o aliyekuwa mpenzi wake.

Eto’o amekanusha kuhusika na mchezo huo mchafu, na katika kujibu mapigo mchezaji huyo anayeongoza kwa kutwaa tuzo nyingi za uchezaji bora barani Afrika, amefungua kesi ya matumizi mabaya ya fedha($410,755) alizompa Ms Koah kwa ajili ya kufungua taasisi ya kusaidia jamii wakati walipokuwa wapenzi.

huyu alishawahi kuwaingiza kwenye beef mwanamuziki Fally Ipupa na Eto’o kwa kuwachanganya kimapenzi.

Welcome to My Blog

Blogger templates

About views Blogger

Mrembo wetu wa leo

KONA YA KIJANJA YA KUJIDA VIA SNAPS

Powered by Blogger.

MY HOT BROGGER TZ

Like My Facebook Page

FOLLOW ME ON TWITTER

Contact Form

Name

Email *

Message *

- Copyright © TIMOKUCHAZ -Robotic Notes- Powered by Blogger - Designed by Johanes Djogan -