Showing posts with label NEWS. Show all posts



Moja ya gumzo kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa ni uwepo wa video fupi inayomuonesha mwananke anayedaiwa kuwa mchawi baada ya kukutwa katikati ya barabara akiwa bila ungo na baadhi ya vitu vinavyodhaniwa vya kishirikina.
Sasa new stori leo leo July 20, 2017 kwenye Hekaheka ya Leo Tena ya Clouds FM mtangazaji Geah Habibu katusogezea hii iliyotokea Kipunguni ambako mwanamke mmoja mwenye mume na watoto alikutwa katikati ya barabara akiwa bila nguo kwa kinachodaiwa ni maelekezo ya Mganga.
Tukio hilo limetokea July 18, 2017 majira ya saa sita mchana ambapo baada ya kukutwa katika hali hiyo wananchi walidhani ni mchawi na wakadhamiria kumchoma moto lakini aliokolewa na Polisi baada ya taarifa kumfikia Mwenyekiti wa eneo hilo…sikiliza full stori kwa kuplay hapa!!!

Moja ya headlines zinazomuhusu mwimbaji sataa wa Bongofleva kutoka kundi la Yamoto Band, Beka Flavour leo July 20, 2017 ni kuhusu kushikiliwa kwake na Jeshi la Polisi DSM kwa mahojiano yaliyodumu kwa saa Tisa kuanzia saa tano Asubuhi hadi saa mbili Usiku.
Ayo TV na millardayo.com zimempata Beka Flavour>>>”Nipo hapa tangu saa tano Asubuhi kwamba natuhumiwa kutapeli pesa za jamaa mmoja kupitia mitandao yangu ya kijamii. Huyu jamaa anaishi Kigoma na anadai kuwa alikuwa akizungumza na mimi na anasema hakuwahi kuonana na huyo Beka basi nilipata taarifa a kuripoti katika kituo hiki na niliporudi kutoka Safari ndio nimelifika hapa.
“Nimetoka kwa dhamana na kikubwa ningependa kuwaomba watu na mashabiki wengi kwamba watu wanaotumia majina yetu sio kitu kizuri kwani kama huyo wa Kigoma aliyetuma pesa anadai ametuma zaidi ya milioni 8. Kwa hiyo, wawe makini na mitandao feki kwani Maromboso, Enoki na wengine hatuna kurasa za Facebook.” – Beka Flavour.
“Kwa sasa nina Manager mpya mbali na Yamoto Band” – Becka Flavour…PLAY kwenye hii VIDEO kutazama kila kitu!!!

Walichokizungumza Star TV baada ya kufungiwa na TRA

Thursday 13 July 2017
Posted by Unknown
Tag :
Mapema leo kulikuwa na stori kuwa TRA Mwanza imeifungia Kampuni ya Sahara Media inayomiliki Star TV, RFA na Kiss FM wakiidai malimbikizo ya kodi ya zaidi ya Tsh. Bilion 4 wakiitaka kulipa ndani ya siku 14 vinginevyo kampuni itapigwa mnada.
Baada ya taarifa hizo Meneja Rasilimaliwatu wa Sahara Rafaeli Shilatu amekiri kufungiwa akidai ni kutokana na malimbikizo ya kodi baada ya uwekezaji mkubwa waliofanya wakati wa kuhama kutoka analogy kwenda Digital ingawa wanajitaidi kuhakikisha kwamba wanarudi hewani na kulipa kodi kama kawaida.
>>>”Lazima tukiri kwamba mmeshuhudia TRA wamefunga maeneo yetu ya kazi na hii inatokana na malimbikizo ya kodi ambayo siyo ya sasa ni ya muda mrefu hata nyie waandishi wa habari mnajua kwamba kadri uwekezaji unavyokuwa mkubwa ndivyo gharama zinazidi kwenye uwekezaji. So, ilitulazimu kutafuta fedha kwenye mabenki ili tuweze kukidhi matakwa ya Serikali ya kuhama analogy kwenda Digatal.
“Niwatoe wasiwasi Watanzania na wapenzi wa Sahara hili ni jambo la muda lakini kampuni yetu inafanya jitihada kuhakikisha kwamba haya yanamalizika vyombo vyetu virudi hewani.” – Rafaeli Shilatu 
Bonyeza Play hapa chini kusikiliza Full story. Source http://millardayo.com/

ROMA MKATOLIKI: SIKUTEKWA KWA SABABU ZA MZIKI

Tuesday 11 July 2017
Posted by Unknown
Tag :
Mwanamuziki Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki” amesema kuwa tukio lililotokea miezi mitatu iliyopita lilikuwa na sababu nyingine zaidi ya muziki anaoufanya, tofauti na watu wanavyodhani.

Roma aliyasema hayo katika mahojiano na EATV kwamba alijua kuwa atawakwaza baadhi ya watu kwa kutosema na kuweka wazi mambo kadhaa kuhusu tukio hilo ikiwemo kutekwa, walipopelekwa, kilichowatokea wakiwa huko walikopelekwa n.k lakini aliamua kutumia busara na kutosema kitu ili aweze kulinda sanaa na maisha yake kwa ujumla.

“Mimi najua nini kilipelekea wale jamaa kututeka. Ni zaidi ya muziki, japo chanzo ni muziki ndio maana walikuja kututeka tukiwa studio na si kanisani wala nyumbani. Unajua wananchi tayari walikuwa na video kichwani wakijua Roma anakuja kuongea hiki na kile, tunamaliza pale halafu usiku mwema.”

“Lile tukio lilikuwa linahitaji busara ili maisha yaweze kuendelea. Labda ningesema ukweli pengine ungekuwa ndio mwisho wa Roma kwenye muziki. Mashabiki wangeshangilia lakini kwa wadau mbalimbali mchango ndio ungekuwa umekwisha,” alisema.
Roma alisisitiza kuwa kama angeweka wazi jambo hilo siku ile ambayo alitoka, ingepelekeaa yeye kuacha muziki na kurudi Tanga kufanya mambo mengine, kwani hakuna mtu ambaye angetaka kuwa karibu naye tena.

“Toka nimetoka mpaka sasa sitaki kutazama video mbalimbali ambazo zinaonesha jinsi watu walivyokuwa wakihangaika kututafuta. Sitaki kutazama kwa sababu sitaki kukumbuka kabisa hali ambayo nilikuwa nayo kipindi kile. Pia sipendi kabisa kuona mtu mwingine yeyote anakwenda huko chimbo ambako tulikuwa tumewekwa tukipata mateso,” alisema.

Roma na wenzake walitekwa mwezi wa nne mwaka huu walipokuwa katika studio za kutayarisha muziki za Tongwe Records na kupelekwa kusikojulikana kwa muda wa siku tatu na kuja kuonekana wakiwa na majeraha mbalimbali mwilini.


Leo June 21, 2017 kupitia XXL ya Clouds FM Mwimbaji staa wa Bongofleva Diamond amezungumzia kwa mara ya kwanza tangu kupost picha na ujumbe kwenye Instagram yake juu mama watoto wake ‘Zari’ kufuatia picha aliyopiga akiwa na mwanaume akiogelea.
Diamond amesema baada ya kuiona picha hiyo alipanic na kuandika ujumbe ule ambao baada ya kusambaa alifuatwa na Zari na alipomuelewesha alimuelewa huku baadhi ya mastaa wa Afrika wakiwepo P Square na Fally Ipupa wakimpigia simu kumpoza hasira.
>>>“Mara ya kwanza nilipoona picha ya Zari kapiga na mtu kwenye maji nilipanic na nilichokiandika kwenye insta yangu nilimaanisha. Baada ya post yangu ya insta wasanii wengi walinipigia simu. P Square na Fally Ipupa walinicheki. Zari baada ya kuona post yangu Insta alikuwa ofisini, alirudi nyumbani na aliponielewesha nilikuwa mpole.” – Diamond Platnumz.
ULIPITWA: Majibizano ya Diamond Platnumz na Zari 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, ameviagiza vyombo vyote vya ulinzi na usalama kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa kuhakikisha vinasimamia sheria ipasavyo ili kukabiliana na tatizo hilo hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Februari, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam, muda mfupi baada ya kuwaapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Rogers William Siyanga, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala, Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mhe. Joseph Edward Sokoine, Balozi wa Tanzania nchini Algeria Mhe. Omar Yusuf Mzee na Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Grace Aaron Mgovano.

Mhe. Dkt. Magufuli amewataka viongozi wote wa Serikali kuungana na vyombo vya dola katika mapambano dhidi ya watu wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya na ametaka mapambano hayo yasifanywe kwa mzaha wala kwa kuangalia majina ya watu, vyeo vyao na taasisi wanazoongoza.

Mhe. Rais Magufuli amewapongeza viongozi wote wa mikoa walioanza kukamata watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na amewaomba Watanzania wote waunge mkono juhudi za kukabiliana na wanaofanya biashara na kutumia dawa za kulevya ambazo zinazidi kuangamiza nguvukazi ya Taifa.

“Niwaombe ndugu zangu tuungane katika vita hii dhidi ya dawa za kulevya, waandishi wa habari na wana mitandao tuweke mbele Utanzania wetu, akitokea mtu anapambana na dawa za kulevya tumuunge mkono badala ya kumchafua.

“Vita hii ni kubwa hatuwezi kwenda nayo kwa mzaha na Serikali itahakikisha inasimamia sheria namba 5 ya mwaka 2015 iliyohusu kuzuia na kupambana na dawa za kulevya ambayo ilitungwa na Bunge la 10 lililoongozwa na Spika Anna Makinda na sheria hiyo ikatiwa saini na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, nawapongeza sana kwa kutunga sheria hii.” Amesisitiza Mhe. Rais Magufuli

Pia, Mhe. Dkt. Magufuli amesema takwimu zinaonesha kuna watanzania 1,007 wamekamatwa na kufungwa gerezani katika nchi mbalimbali baada ya kupatikana na makosa ya kujihusisha na dawa za kulevya, na amemuagiza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi wote wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi hizo kutojihusisha kuwatetea waliofungwa kwa makosa hayo na badala yake waache sheria za nchi husika zichukue mkondo wake.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala kufanya mabadiliko makubwa ndani ya Idara ya Uhamiaji nchini kutokana na utendaji wake kutoridhisha.

“Nataka ukafanye mabadiliko makubwa (Total Reform), nataka Uhamiaji izalishe fedha kwa ajili ya nchi hii, nataka ukadhibiti utoaji hati za kusafiria (Passports) maana zimekuwa zikitolewa hovyohovyo” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao pamoja na kula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela, imehudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Kaimu Jaji Mkuu Mhe. Prof. Ibrahim Juma, Mawaziri, Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

12 Februari, 2017

Miezi kadhaa baada ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kupiga marufuku biashara ya Shisha kwenye sehemu za starehe, ulipita muda na agizo hilo likaonekana kutekelezwa japokuwa haikuchukua muda sana biashara hiyo ikarejea tena.
November 16, 2016 wakati wa uzinduzi wa mitambo ya ufuaji umeme jijini Dar es salaam, Paul Makonda alizungumzia biashara hiyo kurejea kinyemela ikiwa ni pamoja na baadhi ya wafanyabiashara kumfata na kutaka kumuhonga shilingi milioni tano ili wapewe kibali cha kuendelea na biashara hyo.
Makonda amesema kurejea kwa biashara hiyo kunampa mashaka kwamba huenda baadhi ya askari wa jeshi la polisi wamepokea hizo pesa ndiomana wanashindwa kuzuia uuzwaji wa shisha.
Kauli ya  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda imefanya Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda Simon Sirro kutolea majibu kuhusu biashara ya Shisha inayofanyika pamoja na kupigwa marufuku.
“Watu wengi wameshakamatwa pale Oysterbay na majalada yanaandaliwa na mengine yameshapelekwa kwa mawakili wa serikali. Sisi tunaendelea na oparesheni kama kawaida ya kukamata wauzaji, watengenezaji na wavutaji wa shisha” – Kamanda Sirro
Unaweza kutazama video hii kupata majibu ya jeshi la polisi.

NUKUU ZA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI-04

Thursday 8 September 2016
Posted by Unknown
Tag : ,



counter




























Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, ni kiongozi ambaye watanzania tulikuwa tunamsubiri kwa muda mrefu.Mara nyingi anapohutubia huwa anatoa kauli za kufurahisha kwa wapenda maendeleo na kuchukiza wasiopenda maendeleo.
Mtandao huu unakuletea Nukuu za Rais, ambazo zinafurahisha wengi na kuchukiza wachache.





NUKUU 

"Nataka niwaeleze ndugu zangu, serikali hii ya awamu ya tano ipo pamoja nanyinyi, haitowatupa wala haitowabagua, haitowabagua kwa dini zenu haitowabagua kwa makabila yenu na kamwe haitowabagua kwa sababu ya vyama vyenu." 

MAANA YAKE 

Serikali ipo kwa ajili ya kutenda haki kwa raia wote bila kujali dini, kabila au vyama.

Maneno hayo alisema Magomeni, alipowatembelea wakazi waliokuwa wakiishi magomeni kota. Jumanne,06 Septemba, 2016.  

MUANDAAJI. NASSIR BAKARI
OFISI NDOGO ZA CCM
LUMUMBA 
EMAIL: nassiribakari@gmail.com 


Leo ni birthday ya mtoto wa Diamond, Tiffah ambapo ndugu, jamaa pamoja na marafiki katika mitandao ya kijamii wanaendelea kum-wish binti huyo.
Zai

Mmoja kati ya watu ambao wamem-wish binti huyo ni Ex wa Zari, Ivan ambapo amemtakia binti huyo afya njema katika maisha yake. Lakini ujumbe huo umezua upya vuguvugu kwa mashabiki ambao bado wanaamini Tiffah ni mtoto wa Ivan licha ya Diamond kukanusha uvumi huo mara kadhaa.

“Big shoutout to this innocent beautiful soul. May you live to blow more candles to come Princess_tiffah,” aliandika Ivan katika ukurasa wake wa instagram huku akiwa ameweka picha ya binti huyo.

Baada ya kuandika ujumbe huo, mashabiki katika mitandao ya kijamii wamekuwa na maoni tofauti. Haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki hao.

Mtoto karudi kwa baba jaman, Damu nzito nyie @ivandon ongera Ivan kwakupigania mpaka mwanao kaja atimaye mungu mkubwa jaman khaa.

Sweet_verosa
Hahaha yani nimecheka mpaka nimelia eti Mungu mkubwa tifa karudi kwa baba yake.

Didiz_buu
Nimempenda Bure uyu mzungu wa kiganda sijui kisauz…. Big up bro Ivan…. U gat a unique heart… Happy birthday baby teepher

Angellyamuya
Congratulation big Boss I salute you.

Aniveraaaaa
Ivan Don Kai u re a man,dis jst gt me crying a u re a nice man.God will perfect everything dat concerns u and gve h a better companion amen.

Nelyhassan
Sure she is beautiful innocent soul happy birthday girl @princess_tiffah

Cassandra_jolly
Happy birthday to her…..u r a gentleman Ivan

Johnson_willo
Now i realize how gentle ur.@ivandon conglatulation men.And happybornday to the one and only.@princess_tiffah.

Binti_wa_bagoka
My love @christinamboy aiseeee njoo umuone mume wa zari alivyo zungu ametishaaaa

Serikali yataka nidhamu bendera ya Taifa

Thursday 28 July 2016
Posted by Unknown
Tag :

Dar es Salaam. Mpigachapa Mkuu wa Serikali, Cassian Chibogoyo ameonya matumizi yasiyo sahihi ya bendera ya Taifa na wimbo akitaka watendaji kusimamia maadili vinginevyo watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Chibogoyo alisema jana kuwa taasisi hiyo inataka kurudisha maadili na uzalendo kwa wananchi kuheshimu alama za Taifa.

Alisema watendaji wanaopeperusha bendera zilizochakaa na kupauka wanafanya makosa kwani kunaidhalilisha Serikali kwa kuwa mpya zinapatikana bila ya urasimu.

“Baadhi ya watendaji wamekuwa wakiacha bendera zinapeperuka hadi usiku wakati sheria inataka zishushwe saa 12.00,” alisema.

Alifafanua kuwa wananchi wanatakiwa kusimama kwa utulivu wakati bendera ya Taifa inapopandishwa na kushushwa.

“Tofauti na zamani, siku hizi bendera ya Taifa inapopandishwa watu wanapita na kupiga kelele kama vile hakuna jambo linalotokea,” alisema.

Kuhusu wimbo wa Taifa, Chibogoyo alisema haupaswi kuimbwa kwenye vilabu vya pombe bali kwenye mikusanyiko rasmi ya kiserikali.

“Huu siyo wimbo wa kuimbwa ovyo, lazima turudishe maadili yetu Watanzania,” alisema.

Mpigachapa huyo alisema viongozi, watendaji na wananchi wanatakiwa kujifunza na kuufahamu wimbo huo na kuonyesha hisia za kizalendo kwa nchi.


Baraza la madiwani chini ya meya wa manispaa ya Kinondoni Jacob Steven limewachukulia hatua watumishi 18 waliokuwa na tuhuma mbalimbali, watumishi 9 wa uhandisi, 8 afya na 1 wa utumishi fedha na biashara,

Watumishi wa 4 afya wamefukuzwa kazi kwa utoro na rushwa, watumishi 3 uhandisi wamekutwa na hatia kwa kushushwa vyeo na madaraja na mtumishi wa fedha na biashara amepewa onyo kali
uamuzi kwa wahandisi umetokana na wao kushindwa kutumia taaluma zao vizuri kwenye ujenzi wa barabara.
watumishai hao walichukuliwa hatua baada ya kufunguliwa mashtaka, kufanyiwa uchunguzi wa tuhuma zao na wao kupewa muda wa kujitetea.

Baraza la madiwani limewapandisha vyeo watumishi 372, kuwabadilisha vyeo watumishi 9, na kuwathibitisha kazini watumishi 206 ambao walimaliza vipindi vya majaribio na kuonekana kuwa wanafaa kuwa watumishi wa umma

Nawapa hongera kwa kufanya kazi hii kwa weledi na sio kwa show off, wanaofanya kazi kwa show off ili kuonekana wanafanya kazi na wanapenda haki kumbe wana sura mbili wangeiga mfano huu

VIDEO:

Kama hukupata nafasi ya kujua hii baasi kaa ukijua WALTER RWABUKAMBARA ameshamvisha pete VIRGINIA CHIDYAKA

Sasa wako mbioni kuanzisha Family taarifa niliyonayo kwa sasa vikao vinaendelea na michango inaendelea kutolewa

Kama ungependa kuwachangia ili wafanikishe zoezi hili jema wasiliana na Llewellyn Mark kwa namba hizi 0713 697 043


Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajenti Mensah wa Kituo cha Polisi Oysterbay ameuawa usiku huu kwa kupigwa risasi akiwa kazini eneo la Sayansi Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Christopher Fuime amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa mbili usiku huu na chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika.

“Tukipata chanzo itakuwa tayari upelelezi wetu umetimia, hivyo kwa sasa tunalifanyia kazi ili kubaini wahusika wa mauaji hayo,” amesema Fuime.



Aunty Ezekiel alitamani angeenda na mwavuli kujikinga na mvua ya hela iliyomnyeshea juzi kwenye birthday ya kutimiza mwaka mmoja ya mtoto wa Aunty Ezekiel na Mose Iyobo. Ni Diamond ndiye aliyesababisha mafuriko ya noti yaliyomfanya muigizaji huyo apagawe! Check video hiyo ujionee mwenyewe.

1.Rwamkoma Jkt......<<bonyeza Hapa>>

2.Mafinga Jkt .....<<bonyeza Hapa>>

3.Makutupora Jkt.......<<bonyeza Hapa>>

4.Mtabila Jkt......<<bonyeza Hapa>>

5.Kanembwa Jkt.....<<bonyeza Hapa>>

6.Bulombora Jkt.....<<bonyeza Hapa>>

7.Ruvu Jkt.......<<bonyeza Hapa>>

8.Mgambo Jkt ......<<bonyeza Hapa>>
9.Maramba Jkt......<<bonyeza Hapa>>

10.Mlale Jkt.....<<bonyeza Hapa>>

11.Msange Jkt.....<<bonyeza Hapa>>
Baada ya show zake ambazo hazifiki hata 15 toka ametusua kupitia single yake ya Aiyolamkali huyu kutoka WCB ameonyesha bidii ikiwekwa popote kuna matunda. Ni gari aina ya Mark X ambapo Mmiliki wa label ya WCB, Diamond Platnumz alimpongeza na kuandika…’ 

Kama nikusiivyo siku zote ni juhudi na Nidhamu yako ndio itayokufanya upate matunda ya kazi yako….. Usiache unyenyekevu, kuheshimu mkubwa na Mdogo, Kumuomba na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila hatua ndogo Uipigayo…. Congrats kwa your New Ride’ – Diamond


 

Tarehe 1/5/2016 J,pili, David Aliamua kwenda Kanisani Kutoa Shukurani, Ni baada ya Kumpoteza Mama yake Mzazi Kwa Dini za kikristo Ni kawaida kabisa linapotokea jambo kama hilo Kumrudia Mungo wako na Kusema Asante, kwani Tunaimani kwamba kila Linalotokea ni kwa Mipango Yake Mwenyezi Mungu
  





 Kwaya kuu La KKT Ushirika wa Kibo siku hiyo ndio walitoa hudua ya uimbaji
 



 Hapo ni Nyumbani wapishi wakiandaa Mambo ya Misosi 
 










 Baada ya kutoka Kanisani Waalikwa walikuwa Nyumbani kwa ajili ya kupata Chakula
 









































Welcome to My Blog

Popular Post

Blogger templates

About views Blogger

Mrembo wetu wa leo

KONA YA KIJANJA YA KUJIDA VIA SNAPS

Powered by Blogger.

MY HOT BROGGER TZ

Like My Facebook Page

FOLLOW ME ON TWITTER

Contact Form

Name

Email *

Message *

- Copyright © TIMOKUCHAZ -Robotic Notes- Powered by Blogger - Designed by Johanes Djogan -