Ferooz_Ft__Raymond_-_Nimejifunza (Audio)

Thursday, 28 April 2016
Posted by Unknown
Tag :

Najua Ulimiss sana Kuisikia Sauti ya FEROOZ..Sasa amekuletea bonge la Ngoma akiwa chini ya MKUBWA FELLA , Hii ngoma ameshirikiana na RAYMOND kutoka kwa Wasafiii .... Ngoma Hii HAPA ipakueee Mkali wangu

Snura - Chura Dance | Tanzania women Twerking (Official Video)

Wednesday, 27 April 2016
Posted by Unknown
Tag :



This song"FREEDOM"Has Been Produced By Daxo Challi (MJ RECORDS) From Tanzania And Written By SUGU 'The Video Was Directed By Hanscana from Wanene Films.


Itanzame Hapa Video hapa Chini

Ukiona umemtumia mpenzi wako/mchumba wako/mchepuko wako/mke wako au hata rafiki wa kike wakati mwingine SMS ya kawaida tu kwaajili ya kumsalimia lakini yeye akakujibu moja kati ya majibu yafuatayo, tafadhali sana usiendelee kuchat nae maana kinachofuata hapo ni majanga tu.

KWA MFANO: 
1. Ukimtumia sms ''Mambo mpenzi wangu?'' akikujibu ''mambo mabaya'', usimuulize kwanini mambo mabaya, ukimuuliza atakwambia kuwa ''sina hela dear''

2. Ukimtumia sms ''Maisha yanasemaje kipenzi changu'' akikujibu ''maisha magumu hubby wangu we acha tu'' usimuulize kwanini, ukimuuliza kwanini atakwambia ''nimefulia mwenzio kama nini sijui''

3. Ukimtumia sms ''Mbona kimya sana mchumba wangu, umenitupa kiasi hicho'' akikujibu ''sijakutupa wangu yaani mambo hata hayaendi'' usimuulize kwanini mambo hayaendi, ukimuuliza atakwambia kuwa ''yaani sina kitu mpenzi wangu, simu ilikuwa haina hata hela ya kubeep''

4. Au ukiona mwanamke anaanza kwa kukwambia nikwambie kitu? We mkatalie kiutani utani tu, mwambie usiniambie, hata akikomaa vipi akwambie mwambie sitaki uniambie huku unafanya kama utani lakini moyoni unakuwa upo serious.

Ni mara chache sana mwanamke akikwambia kuwa mambo mabaya, maisha magumu au mambo hayaendi huwa na matatizo mengine kama kuumwa, misiba.... n.k lakini THE REST ni wapigaji mizinga tu. Akikwambia maisha magumu mjibu ''pole wangu, mambo mengine vipi?''

Ukipewa majibu kama hayo, chagua moja, either usiendelee kuchat nae mpaka badae kidogo au mbadilishie maada ili kukwepa huo mzinga ambao unakuja mbele yako.

New Video: Lady Jaydee – Ndindindi

Tuesday, 26 April 2016
Posted by Unknown
Tag :
Lady Jaydee ametoa maana ya wimbo wake ‘Ndindindi’ ambalo lilikuwa ni fumbo lililokuwa linawapa majibu mengi yasiyokuwa na uhakika mashabiki wake.

Wimbo wa ‘Ndindindi’ unazidi kufanya Vizuri kwenye medi mbalimbali na kumrudisha vizuri Jide aka Binti Komando kwenye muziki wa Bongo Fleva baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuachia wimbo wowote.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Lady Jaydee alisema, “The Ndi mimi ni kitu tori wewe si kitu” lakini pia aliongezea “ili kuleta fleva ya muziki ndiyo nikaiita Ndindindi. Mimi ni kitu na wewe si chochote.”


RC Makonda katangaza kuwaondoa Wakurugenzi..(+Video)

Sunday, 17 April 2016
Posted by Unknown
Tag :

April 17 2016 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alikutana na waandishi wa habari na kuzungumzia baadhi ya changamoto zinazoendelea katika jiji lake ikiwa ni pamoja na vitendo vya matumizi mabaya ya fedha yanayofanywa na baadhi ya viongozi,  Makonda anasema>>

Kwenye mkoa wetu wa Dar es salaam tuna mambo ambayo yamekuwa yakiendelea ambayo yamekuwa yakikiuka sheria, kanuni  na taratibu, moja ya vitu vilivyobainika katika stendi ya ubungo imebainika kwamba Meneja anatumia sharia ya mwaka 2004 kulipa mapato, wakati sharia inayotambulika kwa sasa ni sharia ya mwaka 2009

Mkataba wa mwaka 2009 kwa mwezi tunapaswa kukusanya si chini ya mil 84, wakati wa mwaka 2004 tunakusanya mil 42 kwa mwezi, manaake tunapoteza mil 42 kwa mwezi

Hapa inamaana kwa mwaka ni zaidi ya Milioni 500 zinapotea, na ukiangalia kuanzia mwaka 2009 tumepoteza jumla ya Bil 3, ajabu waliosaini mkataba wa tarehe 30/01/2015 ndio walewale waliosaini tarehe 31/01/2015

Lakini pia ishu ya maegesho ya magari haijampita Makonda, na anasema ‘Upande wa maegesho ya jiji inaonekana mzabuni tenda yake ilikwisha muda wake, chaajabu haikutangazwa tenda bali akaandikiwa barua ya kuongezewa muda, jambo ambalo halipo kisheria

Sasa hapa inaonekana kuna uhusiano mazuri sana kati ya wanaokusanya pesa na wale wanaopokea, na watu hao ni viongozi

Vipi kuhusu ishu ya bodaboda? Makonda anasema ‘Faini ya makosa ya pikipiki ni shilingi elfu 20, lakini Tambaza anawatoza watu elfu 80, imefika hatua wanakatazwa kumkamata mtu bila kujieleza, lakini kinachofanyika ni kinyume na taratibu

Hawa Wakurugenzi ambao ambao badala ya kutusaidia sasa wameamua kutuangamiza, nimeiomba mamlaka husika ya nidhamu ichukue hatua stahiki, mimi kwenye mkoa wangu siwahitaji kuendelea kuwanyonya wana Dar es salaam
Roma Mkatoliki ni msanii maarufu wa hiphop Tanzania ambaye kwenye upande wa pili wa maisha ameamua kufunga ndoa na mpenzi wake wa longtime ambaye wana mtoto pamoja (Ivan) na April 9 2016 ndoa imefungwa nyumbani Tanga na ni baada ya send-off kufanyika Dar es salaam February 2016.

roma 5

Roma 4

Roma 2

February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.
February 2016 kwenye send-off Roma Mkatoliki akisindikizwa na mshkaji wake Kala Jeremih.  Hip Hop Tz


Huduma ya WhatsApp haitatumika tena katika simu zinazotumia mifumo kadha ya programu ikiwemo Blackberry 10, Nokia Symbian S60 na Windows Phone 7.1.

Kampuni ya Facebook inayomiliki huduma hiyo imesema inataka kuangazia kustawisha “huduma katika mifumo inayotumiwa na watu wengi.”

WhatsApp, itaacha kufanya kazi katika mifumo hiyo ya programu kufikia Desemba 2016. Licha ya kuacha kutumika katika simu nyingi za Blackberry, WhatsApp bado itaendelea kutumiwa katika simu za kisasa zaidi za Blackberry kwa sababu simu hizo hutumia mfumo wa Android.

Kampuni hiyo imejitetea na kusema kwamba haijawatupa wateja wake ambao wamechangia sana katika ufanisi wake lakini ni kutokana na mabadiliko ya teknolojia.

“Simu hizi hazina uwezo wa kiteknolojia tunaohitaji kuendelea kuimarisha huduma yetu siku zijazo,” kampuni hiyo imesema.



Orodha kamili ya mifumo ya simu ambayo wateja hawataweza tena kutumia WhatsApp ni hii hapa:
Android 2.1 and Android 2.2

Blackberry OS 7 and earlier

Blackberry 10

Nokia S40

Nokia Symbian S60

Windows Phone 7.1

Kampuni hiyo imesema wakati wa kuanzishwa kwa WhatsApp mwaka 2009, asilimia 70 ya simu wakati huo zilikuwa za BlackBerry na Nokia.”

Lakini sasa asilimia 99.5 ya simu zinatumia mifumo ya Google, Apple na Microsoft.

Source: BBC



Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli, April 5 2016 jina lake limerudi kwenye headlines kwa mara nyingine tena. Rais Magufuli amerudi kwenye headlines baada ya kukubali mwaliko wa Rais Paul Kagame wa Rwanda, hivyo atafanya ziara ya siku mbili Jumatano na Alhamisi.

Stori kutoka wizara ya mambo ya nje zinaeleza kuwa Rais Magufuli pamoja na Rais Kagame watafungua daraja la kimataifa la Rusumo linaounganisha mpaka wa Tanzania na Rwanda na kuzindua ushirikiano wa huduma za kituo cha pamoja.Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari na kusomwa katika television za Tanzania Rais Magufuli atasafiri kwa gari.

2
Kutoka kushoto ni Rais Magufuli na Rais Paul Kagame wa Rwanda
Rais Magufuli pia atakwenda kuweka shada katika makaburi ya mauaji ya Kimbali ya mwaka 1994 na baadae kufanya mazungumzo ya pamoja na Rais Kagame mjini Kigali. Hii ndio itakuwa safari ya kwanza ya Rais Magufuli kusafiri nje ya nchi toka aingie madarakani October 2015.
Van Jack  a.k.a Arsene_Wenger wemgi ndivyo wanavyomuita hivyo pande za Ubungo jijin dar Tanzania Ni maarufu sana pande hizo hidi Snaps company Imeamua kumpa offer ya Picha Hii Unaweza ukamfollow kwa link hizi    Facebook     Instagram   Kama na wewe Unahitaji utokelezee na Chama lako wasiliana nasi kwa
 Whatsapp 

Itazame Michoro yetu kwa video hii hapo chini

kwa Maoni na Ushauli unaweza wasiliana nasi kwa simu no +255713624383 au unaweza ukatu follow kwa link hizi          Facebook    Instagram    Twitter
 Binti akiwa na Shanga wazee wa zamani wanasema huyo ana adabu Hilo jambo kweli linamaana Japo sina uhakika Wadada wa Leo wanazitumia Vizuri hizo Shanga


Hebu itazame hii Video Hapa

Videos


Usichukue muda kujiuliza mara yako ya mwisho kutazama video mpya ya Mh. Temba ilikua lini? right now yuko kwenye spika zetu na hii single inaitwa ‘fundi’ na ukishatazama usisahau kuniachia comment yako hapo chini ili Temba akipita hapa ajue mashabiki wake wameipokeaje.



Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.


Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa.


Bei mpya  kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292  toka  298  ya  zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200  ya  hapo  awali.

Bei mpya  kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152  toka  sh. 156  ya  hapo awali


 
 
Licha ya jitihada za serikali kutangaza vita dhidi ya wauzaji na wanunuzi wa miili ya kinadada na kuwataka waache kwa kuwa ni kinyume cha maadili na sheria ya nchi, warembo hao (sio walio pichani ukurasa wa nyumawamedaiwa kukaidi agizo hilo huku wakidai kama aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf Makamba alishindwa basi hata mkuu mpya wa mkoa huo, Paul Makonda hatawaweza.

Hivi karibuni, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Simon Sirro alitangaza oparesheni maalum ya kuwasaka madada poa hao, sambamba na wateja wao akidai wanakiuka sheria na maadili ya Mtanzania jambo ambalo liliungwa mkono na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
Mara baada ya agizo hilo la serikali kutolewa, wanahabari wetu walifanya uchunguzi katika maeneo ambayo yamezoeleka kwa biashara hiyo na kukuta baadhi yao wakiendelea kama kawaida kana kwamba hakuna agizo lolote lilitolewa.

Risasi lilipita maeneo ya Sinza-Mori jijini Dar na kuwakuta akina dada hao wakiendelea na biashara hiyo kwa kujipanga barabarani kuelekea baa maarufu ya Meeda ambapo wanahabari wetu waliojifanya wateja walipowauliza kulikoni hawaogopi nguvu ya dola, walisema wao wameshindikana tangu enzi za Makamba, Kandoro na Said Meck Sadick (aliyepita) hivyo hata huyu wa sasa, Makonda hatawaweza.

Wewe hii ni nguvu ya soda. Hatuwezi kuacha unafikiri tutakula wapi? Hii kazi tumeanza kitambo, tangu enzi za Makamba aliyekuwa hatari kweli kukemea biashara hii lakini tulimshinda. Akaja Sadick naye tukamgaragaza sembuse huyu Makonda aliyepewa jiji hili juzi tu?” alisema dada poa mmoja aliyekataa kutaja jina lake.

Maeneo mengine ya Jiji la Dar ambayo Risasi lilibaini kuwa biashara hiyo bado inaendelea kama kawaida ni pamoja na Sinza-Afrikasana (maarufu kama Conner Bar), Buguruni (Kimboka Bar, Rozana), Temeke na Kinondoni-Makaburini.

Alipotafutwa Makonda kuhusiana na suala hilo alisema atalizungumza kwa kirefu baada ya Sikukuu ya Pasaka lakini mwanahabari wetu alipombana zaidi ili aweze kutoa ufafanuzi kwa kuwa madada poa hao wamekaidi agizo la serikali, aliahidi kulizungumzia siku iliyofuata (Machi 21) lakini hata hivyo siku hiyo alipopigiwa simu hakupokea.


Hata mwandishi wetu alipomtumia ujumbe mfupi wa maandishi kumsisitiza azungumzie suala hilo, Makonda hakujibu chochote.

Aidha, mwandishi wetu pia alimtafuta Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro ili aweze kuzungumzia suala hilo, aliomba atafutwe baadaye kwa kuwa alikuwa kwenye kikao. Baadaye simu yake haikupatikana hewani.

GPL


Rais John Pombe Magufuli aliwateua wakuu wapya wa mikoa Tanzania bara March 13 2016 ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, watano wamehamishwa vituo vya kazi na mmoja amepangiwa Mkoa mpya wa Songwe sasa wakati wa kuwaapisha kuna mmoja wa viongozi aliteleza kufata kanuni za viapo, tazama kwenye hii video hapa chini.


Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars March 23 imeshuka katika dimba la Idriss Mahamat kucheza na wenyeji wao timu ya taifa ya Chad katika muendelezo wa michezo ya makundi ya kuwania kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika  (AFCON) itakayochezwa mwaka 2017.

Huu ulikuwa ndio mchezo wa kwanza wa Mbwana Samatta akiichezea Taifa Stars kama nahodha wa timu hiyo, katika mchezo huo uliochezwa Chad, Taifa Stars imeibuka na ushindi wa goli 1-0, goli la Taifa Stars lilifungwa na Mbwana Samatta dakika ya 30, baada ya kutumia vyema krosi ya Farid Musa.

Samatta amefanikiwa kuitunzia Tanzania rekodi dhidi ya Chad, kwani mara ya mwisho Taifa Stars alikutana na Chad, ugenini na kufanikiwa kuibuka kwa ushindi wa goli 2-1. Magoli ya Taifa Stars wakati huo yalifungwa na Mrisho Ngassa dakika ya 11 na Nurdin Bakari dakika ya 88, huku goli la Chad la kufutia machozi lilifungwa na Mahamat Labbo dakika ya 12.
raaaa
Msimamo wa Kundi G ulivyo hadi sasa
Taifa Stars itarudiana na Chad Jumatatu ya March 28 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam, huku ikiwa imebakiza mechi mbili dhidi ya Nigeria ugenini na timu ya taifa ya Misri utakaochezwa uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.


Mtangazaji wa Clouds FM, Diva amesema Chidi Benz atamsaidia kuandika mashairi ya wimbo wake mpya alioupa jina ‘Kosa Langu.’

Kupitia Instagram, Diva amedai kuwa Mr Blue pia atahusika kwenye wimbo huo mpya unaovunja kimya chake cha zaidi ya miaka miwili kwenye muziki.

“@lamarfishcrab vibin this weekend , Nilikutana na Chid Benz Juzi, akaniahidi kuniandikia wimbo na Kusisitiza ndani ya Mwezi huu nifanye RNB Moja amazing,” ameandika Diva.

“Sometimes kuimba inahitaji hisia sana, hapa kati nimekubwa na misukosuko ya Mapenzi nikaumia sana , and i said why nat Put this into a love song … yes nikapata melody and the verse and chorus Paw jus like that .. called Lamar like YOH ‘ ts about time .. lets jus do the hook up, am very comfy when it comes to studio session with Lamar , matter fact ts been a while and me and blue this year tulikaa and discuss the return,” ameongeza.

“Then nikaanza andika , wimbo wangu verse ya Kwanza nimeandika Mwenyewe , Verse ya Pili itaandikwa na Chidi Benzi and Mr Blue Bayser atamalizia Na Rap Music , strictly RNB ‘ Leo usiku tunaanza kazi ya Kurekodi wimbo Unaitwa ‘ Kosa Langu ‘ saa 6:15 usiku , Production ya Fishcrab Cook Out. Utakuwa ni wa Kiswahili kilichounganika na kiingereza, a very beautiful song wish muuskize and Utatoka week 2 Mbele, after a week itakuja video then …

kuusambaza All over Africa , so stay Tuned, always been a fan of Chidi and Mr. Blue, Very Talented…. But Kosa Langu is jus tooo emotional , huwezi amini i crieeed wakati naandika , trials and tribulations , love this and that but sucha happy song , Extremely.”

“I believe in Chiddi Benz Chuma, I believe in his Talent as well , amenisisitiza sana Kufanya this song .. and y’all kno me i live it to the fullest and always givin a shot .. i live to Please My heart … And wanna Be Happy man, Music is the way forward ya Happiness , This time hits me to the core .. and i can’t deny it ama go with The flow YO… lemme.”

Kabla ya hapo Diva aliwahi kuachia wimbo Piga Simu aliomshirikisha Diamond na Mgonjwa kwa raha zako aliomshirikisha Mr Blue.



KUFURU! Mama wa staa mwenye jina kubwa Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasimu ‘Sandra’ amedaiwa kufanya kufuru ya aina yake kwa kununua mtaa mzima, Tandale-Uzuri jijini Dar na kuikarabati nyumba yake aliyokuwa akiishi zamani kwa kutumia takriban shilingi 100 Milioni

Chanzo chetu makini ambacho kilifuatilia ishu nzima tangu nyumba hiyo ilipoanza kukarabatiwa, kimesema kwamba kwa kipindi kirefu ‘bi mkubwa’ huyo amekuwa akifika nyumbani hapo asubuhi na kuondoka jioni akisimamia ujenzi sambamba na binti yake, Esma.


 Nyumba hiyo kabla ya kukarabatiwa.


“Mama Diamond noma, kateketeza shilingi milioni 100 na bado nasikia ameshafanya mchakato wa kununua nyumba za jirani ili mtaa mzima uwe wao,” kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kimezidi kutiririka kuwa mama Diamond anataka kuifanya nyumba hiyo kuwa bora zaidi kwani mbali na kuiboresha, kuna mpango wa kutengenezwa swimming pool (bwana la kuogelea).

 Ikiwa inakarabatiwa


Mara baada ya kupenyezewa ubuyu huo, gazeti hili lilifika kwenye nyumba hiyo na kuzungumza na mama Diamond aliyekuwa bize kusimamia ujenzi.



“Jamani! Taarifa hizi mmezitoa wapi tena? Kweli nimekarabati nyumba yetu iwe bora zaidi. Hayo mambo ya gharama na mipango mingine ni siri labda mje mmuulize Diamond akirudi Marekani lakini ukarabati huu mnaouona ndio nimeusimamia mimi na mwanangu Esma,” alisema mama Diamond.
Imekuwa Kama Kawaida kumsikia Roma akiiba Nyimbo za Siasa Lakini leo Hii kaja na Hii Bonge la Wimbo wa Mapenzi Hivi ulikuwa unajua kama Roma anajua Kubembeleza.

 Hebu fanya kuusikiliza hapa Wimbo wake Mpya
 Song _ Mtoto wa kigogo

Welcome to My Blog

Popular Post

Blogger templates

About views Blogger

Mrembo wetu wa leo

KONA YA KIJANJA YA KUJIDA VIA SNAPS

Powered by Blogger.

MY HOT BROGGER TZ

Like My Facebook Page

FOLLOW ME ON TWITTER

Contact Form

Name

Email *

Message *

- Copyright © TIMOKUCHAZ -Robotic Notes- Powered by Blogger - Designed by Johanes Djogan -